Monday, July 1, 2013

Mr. & Mrs. Joe.....wamefika Tanzania......

 Leo nimepata suprise, mrs. Jossyanne amekuja tayari, kumbe tokea ijumaa, sasa wakawa wanataka kunifanyia suprise, mdogo wake akanipigia simu akaniambia, ananiletea mteja mchana.. Haya nikajiandaaa, na kuja ofisini kuja kusubiria mteja.......Hee mara anaingia na Jossyanne....yaani nilifurahi mnooooooo. mpaka nikashindwa kuongea kwa muda tumebaki tumekumbatiana........na mumewe nae tukasalimiana, yaani hua ananicheka, kua nina mwili mdogo, basi hua ananibeba, ananiambia jamani uko hivi hivi kila siku......hahhaahahhahaha.....

Wako ofisini kwetu, na wakitizama rangi za Dulux color chart yetu......na tukaongea mawili matatu........

Mimi na Jossyanne tumejuana kupitia blog... mwaka ule ule nioanzisha blog mwezi 8 mwaka 2009.   Alinipigia simu na kusifia ninachokifanya, na tukawa tunawasiliana mara kwa mara.....na mwisho wasiku, tumekua ni ndugu, sio marafiki sasa.......

Tunashauriana, maisha, biashara etc......blog imeniletea marafiki, na wengine wamekua ni ndugu sasa......

Yeye ndie mama wa ubatizo wa Jaydan wangu......

NB:
Mrs, Jossyanne ataanza kupatikana kikazi kuanzia tarehe 20/7/2013   karibuni mtoe appointment, na muweze kusaidiwa katika swala la gardening & landscaping in a proffessional way.........

HOMEZ DECO INAWATAKIA MAANDALIZI MEMA YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN.....

 Siku ya tarehe 30/06/2013 ambayo ni jana, kulikua na mkutano wa wanawake wa kiislam, na pia kulikua na maonesho ya biashara, tunashukuru Mungu nasi Homez Deco tuliweza kuwepo katika hili, na tukauza pia baadhi ya vitu, na mimi binafsi nilipata mawili matatu, katika mawaidha......

Mimi Sylvia Namoyo, baba yetu alikua ni Muislam, na mama alikua ni Mkristo, nimetumia wakati uliopita, maana wazazi wote wako mbele ya haki, na Mungu amewapenda zaidi.

Nimelelewa katika malezi ya ukristo na mama mdogo......maana tuliachwa tukiwa wadogo.....mimi ni mtoto wa 4 wa marehemu Said Namoyo.

Kwa kweli ninamshukuru sana sana sana, mama yangu mdogo, ambae kwa kipindi hichi chote amenilea, na kunisomesha, na kuchukulia kama mtoto wake wa kumzaa mwenyewe, sijawahi pata mateso yoyote yale.
Mama yangu huyu anastahili pongezi sana sana, maana yeye ndie alienipa ujasiri na anaendelea kunipa ujasiri mpaka hii leo, nina biashara yangu, maisha yangu, mtoto wangu. na vyote hivi navimudu mimi mwenyewe.

Malezi aliyonipa mama yangu, ni yale ya kujitegemea mwenyewe, na si kutegemea cha ndugu ama mtu. Nikiwa nacho nashukuru Mungu, nisipokua nacho pia nashukuru Mungu, na ninaendelea kuongeza bidiiii....

Amenifunza mengi nikiwa mdogo, ingawa saa ingine akili za utoto unaona kama vile mmmmmhh, leo mama kapitiliza, ila sasa najionea ukweli wake, kua asingefanya vile, ningeaibika hapa duniani, na ningekua ni mzigo kwa kweli.

Siku ya jana ndio mara yangu ya kwanza kuvaa ushungi, kama ninavyoonekana, hua ninafunika tuu kichwa ilimradi, lakini kufunga kama inavyotakiwa ilikua ni jana.....

Kwa sekunde kadhaa, nilimkumbuka baba.....katika vazi hili.....ila ndio hivyo....Mungu amempenda zaidi.

Nawaombea Mungu aendelee kuziweka roho zenu wazazi wangu peponi......Amin. Tunawakumbuka sana sana.


Namuombea Mungu pia mama yangu aendelee kumpigania na kumuombea maisha marefu hapa duniani, maana yeye ndio kimbilio langu kwa hapa duniani, mimi na Jaydan wangu......

NB:
Kwa wale wote wanaolea watoto wa ndugu zao, kaeni nao vizuri, watunzeni, wasomesheni, kama watoto wenu, maana hamjui siku za mbele atakua nani, na ukute yeye ndie atakae kuja kukusaidia baadae.


Wallpaper kwenye ukuta unaokaa TV, sitting room...........

 Matumizi ya wallpaper kwenye nyumba zetu. Wallpaper ni karatasi za urembo, ambazo ni maalum kwa kuwekwa ukutani, na zinabandikwa na gundi, ziko za aina nyingi, kuna za aina nyingi, za bafuni, jikoni, hizi ni tofauti, na kuna za sitting room na chumbani hizi zinatumika kote kote.


Hizi picha ni mifano ya wallpaper inavyoonekana ikiwa imeshawekwa, na wallpaper ziko za rangi tofauti tofauti, na utahitajika kununua wallpaper iendane na fanicha zako ama rangi zisipishane sana, la sivyo kutachusha, na kuchukiza. Mwanga pia ni wakuzingatia, ili wallpaper iweze kuvutia na kuongezeka na kua na mvuto.
 Kitu kingine ni kua wenzetu wakiweka flat screen tv ukutani, huoni nyaya zikining'inia, na hii nitakuja kulizungumzia hivi karibuni, kwani utakuta nyumba zingine, nyaya nyingi zaidi, zina ning'inia na hakupendezi....
 Wallpaper hubadilisha muonekano kwa haraka na ni nafuu. maana unabandika na haziharibu ukuta. bandika kwenye ukuta wa tv, na kwenye kuta zingine, rangi inaendelea kubaki, ama






karibuni kwa mahitaji ya wallpapers......bado sale inaendelea @ roll 50,000/- na ina urefu wa mita 10 na upana 53 cm.